• MISEMO

    Monday, March 6, 2017

    Usimshauri mtoto wako kufanya siasa, huu mchezo unahitaji… – Mrisho Mpoto

    Msanii mkongwe wa muziki wa asili, Mrisho Mpoto amewataadharisha wazazi kuacha kuwashauri watoto wao kuingia kwenye siasa.
    Mtunzi huyo mahiri ya mashairi ya Kiswahili ambaye aliwahi kutajwa na vyombo vya habari kutaka kugombea ubunge katika uchaguzi iliopita wa mwaka 2015, amekuwa akichambua baadhi ya matukio yanatokea nchini.
    Jumatatu hii ameibuka na kuwashauri wazazi kuacha kuwashauri watoto wao kuingia kwenye siasa kwa madai siasa siyo ishu ya lelemama.
    “Hizi ni salaam zangu kwa kina mama wote wenye watoto tumboni, na wale waliokua leba. Pls pls wakijifungua naomba wasiwashauri watoto wao kufanya siasa huu mchezo unahitaji uwe na roho ngumu kama za wale #shilawadu,” aliandika msanii huyo Instagram.
    Mwanamashairi huko mbioni kuachia project yake mpya.

    No comments:

    Post a Comment

    Fashion

    Beauty

    Culture